Breaking News
recent

ENEWZ AFRICA | Ray Vanny kuja na ngoma aliyomshirikisha Diamond



Good News kwenye muziki wa Bongo Fleva wiki iliyopita ni Ishu ya watanzania Diamond Platnumz,Alikiba na Navy Kenzo kushinda tuzo za Hipipo Music Awards huko Uganda. Moja ya tuzo alizoshinda Diamond ni tuzo ya Video bora East Africa kupitia video ya Salome aliyomshirikisha msanii wa label yake, Ray Vanny.
Baada ya ushindi huo, Raymond amefunguka kuhusu kufanya tena ngoma Na Diamond ambapo amedai kuwa itakuwa ni ngoma yake yeye. “Lazima,watu wasubiri,” amesema Ray kupitia Supermega ya Kings Fm.
Tayari Rich Mavoko na Harmonize wamemshirikisha bosi wao huyo kwenye nyimbo zao, Kokoro na Bado.

No comments:


Powered by Blogger.