Breaking News
recent

Dogo Janja anazeeka vibaya, asaidiwe – Nedy music

Msanii wa muziki kutoka label ya PKP ya Ommy Dimpoz, Nedy Music anaendelea kushambuliana na rapa Dogo Janja kutoka Tip Top Connection.


Nedy Music
Mzozo huo ulianza baada ya rapa huyo kujinadi kwamba yeye ni mkali wa kuvaa kuliko wasanii wote kauli ambayo ilipingwa na muimbaji huyo wa ‘Dozee’ kutoka PKP.
Akiongea na Bongo5 Jumatato hii, Nedy amedai Dogo Janja ni kama mzee ambaye anazeeka huku uwezo wake wa kufikiri ukipungua kila siku.
“Mimi nachoweza kusema ni kwamba Dogo Janja asaidiwe, ana zeeka vibaya kila siku anabadilika,” alisena Nedy “Uwezo wake wakufikiri unapungua kila siku, mimi ningewashauri ndugu zake wamsaidie kwa sababu anapotea,”
Aliongeza, “Pia Dogo Janja amefundishwa kuvaa na Madee hakuna asiyejua hilo, tena ananunua nguo za Manzese, hawezi kushindana na mimi labda ashindanishwe na densa wangu lakini siyo mimi mtoto wa mjini,
Nedy kwa sasa anafanya vizuri na wimbo, Dozee.

No comments:


Powered by Blogger.